IQNA

Chuki dhidi ya Uislamu

Mmarekani Yahudi aliyeivunjia heshima Qur’ani  ashtakiwa kwa jaribio la mauaji dhidi ya jirani Muislamu

18:39 - August 17, 2024
Habari ID: 3479288
IQNA - Mwanaume Myahudi, Izak Kadosh wa eneo la Brooklyn, Marekani anakabiliwa na mashtaka zaidi ya 40, ikiwa ni pamoja na jaribio la pili la mauaji na uhalifu wa chuki, kutokana na vitendo vyake vya chuki  dhidi ya jirani yake Muislamu, Ahmed Chebira.

Malalamiko ya jinai yanasema kuwa vitendo vya Kadosh vilichochewa na tofauti za kidini na kikaumu. Kadosh alidaiwa kutishia kuingia katika nyumba ya Chebira na kumuua kwa sababu ya imani zao tofauti.

Alikamatwa siku ya Jumamosi, siku mbili baada ya kuripotiwa kuvunja nyumba ya Chebira, kuiharibu, na kuivunjia heshima Qur’ani Tukufu.

Siku hiyo hiyo, Kadosh alidaiwa kumpiga Chebira kichwani na panga na kumsababishia majeraha makubwa yaliyohitaji kulazwa hospitalini.

Chebira, ambaye alihamia katika jengo hilo mnamo Oktoba, aliripoti kuwa unyanyasaji huo ulianza muda mfupi baada ya kuwasili kwake. Alieleza kufarijika kwa kukamatwa kwa Kadosh, akihofia mashambulizi zaidi baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini.

3489525

Malalamiko hayo yanaelezea matukio ya mwanzoni mwa Machi, ikiwa ni pamoja na kukatwa kwa matairi, uharibifu wa milango, kushambuliwa kimwili na vitisho vya mara kwa mara kwa maisha ya Chebira.

Kumekuwa na hali tete katika visa vya chuki dhidi ya Uislamu kote Marekani na nchi nyingine kadhaa za Ulaya Oktoba mwaka jana wakati utawala katili wa Israel ulipoanzisha vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.

3489525

Habari zinazohusiana
captcha